WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

.

.

.

.

.

.

MUDATHIR YAHYA

MUDATHIR YAHYA

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

SEIF ABDALLA "karihe"

SEIF ABDALLA "karihe"

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

www.ofaznz.net

Total Pageviews

Wednesday 2 September 2009

TANZANIA YASHUKA NAFASI MOJA KATIKA KIWANGO CHA SOKA DUNIANI

Tanzania imepokezana nafasi na Albania katika ubora wa soka duniani baada ya Albania iliyokuwa chini ya Tanzania ikiwa nafasi ya 94 kupanda nafasi iliyokuwa Stars ya 93 na Taifa Stars kushuka nafasi ya 94 licha ya kushinda mechi yake ya kirafiki dhidi ya Rwanda hivi karibuni,
kulingana na kiwango cha soka cha Rwanda hakikuweza kuisadia Tanzania kupanda juu mbali na kushinda mechi hio ambapo kiwango huangaliwa kulingana na uzito wa nchi pinzania,
kwa maana hio Tanzania inahitajia kujiweka tayari kuathirika tena kidogo na kuporomoka zaidi kutoka nafasi iliyokuwepo sasa baada ya kutokuwa na mpango wa kucheza mechi yoyote ya kirafiki kwa wiki hizi zijazo,wakati nchi nyingine zikiwa na mechi za kuwania nafasi ya kwenda south Africa/angola au kucheza mechi za kirafiki.
tunatarajia Tanzania itapata somo kidogo la kutopoteza kupata nchi za kucheza nazo kwa kufanya matayarisho mapema na kupata mechi za kirafiki kila kutakapokuwa na kalenda ya fifa ya mashindano au mechi za kirafiki.
pamoja na matokeo hayo ni Uganda pekeyake ndio iliyokuwa juu ya Tanzania kwa kuwa katika nafasi ya 72,
kenya ipo nafasi ya 104,malawi 105,Rwanda 117,Congo DR 118, Sudan ambayo kwa miaka mingi ilikuwa juu ya Tanzania kwa soka duniani imeporomoka hadi nafasi ya 96.
-------------------------------------------------------------------------------------------------