Kocha msaidizi wa timu ya Taifa ya Sweden Mr Bo Nilson alikuwepo nchini hivi karibuni akiwa na vijana oranje football Academy,(pichani) Mr Nilson akiwaelekeza chipukizi wa Oranje Football Academy katika kiwanja cha mao-tse-tung.
Kocha Nilson ambae amenyanyua viwango vya wachezaji wengi wa soka nchini Sweden akiwemo nyota Zlatan Ibrahimovic wa timu ya Taifa ya Sweden na F.C Berçalona ya Spain,
akiongea na vijana hao wa O.F.A mr Nilson alisema katika nyota ambao anajivunia zaidi katika matunda yake ni Zlatan Ibrahimovic ambae amekuwa akitamba na kuonyesha kiwango cha juu cha soka kila timu anayochezea ambapo alianza ufungaji wake akiwa katika timu ya Ajax Amstedam ya Holland kabla ya kuhamia Inter Milan na baadae kujiunga na mabingwa hao wa Ulaya Berçalona.
kituo cha kukuza soka kwa vijana nchini cha Oranje Football Academy kipo katika mipango mingi ya kuwasaidia nyota wake kuweza kupata mafunzo kutoka katika makocha mbalimbali wa nje ili kuwaendeleza vijana hao kisaikologia pamoja na kuwajenga katika mfumo mzuri kwa faida ya Taifa hapo baadae.
.........................................................................................................................................................................
.........................................................................................................................................................................
Executive Board begins with a focus on the new UNICEF Strategic Plan,
2018–2021
-
NEW YORK, United States of America, 7 February 2018 – The UNICEF Executive
Board opened its first regular session yesterday, welcoming its new
President fo...
6 years ago