Habari zaidi zimesema kuwa nyota huyo alikwenda Real Madrid kuziba pengo la mfungaji wao kutoka Argentine Gonzalo Higuain ambae aliumia na sasa amerejea tena katika kikosi hicho na ameonyesha maendeleo makubwa kila siku ambapo viongozi wameridhishwa na mshambuliaji wao na hivyo kutohitaji kumnunua Adebayor kuziba nafasi hio.
Wakati huohuo tayari Uongozi wa Bayern München ya Ujerumani imeanza mazungumzo ya kumuwania mshambuliaji huyo wa Manchester City ili kuimarisha kikosi chake kwa msimu ujao ambapo pia wanataraji kumuacha mfungaji wao Miroslav Close.