WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

.

.

.

.

.

.

MUDATHIR YAHYA

MUDATHIR YAHYA

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

SEIF ABDALLA "karihe"

SEIF ABDALLA "karihe"

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

www.ofaznz.net

Total Pageviews

Saturday 7 May 2011

CAF CHAMPIONS LEAGUE

Katika mashindano ya Caf Champions League leo kutakuwa na pambano moja kati ya Enyimba ya Nigeria mbao ataikaribisha Ittihad ya Libya baada ya pambno la kwanza kutoweza kufanyika kutokana na matatizo ya kisiasa yanayoendelea nchini libya,hivyo mshindi wa leo ataweza kusonga ktk hatua ya mini-league,mpaka hivi sasa mabao ni 0-0 na kama watatoka sare ya kuanzia bao 1-1 basi Ittihadi itasonga mbele kwa kuhesabiwa bao la ugenini hivyo pamoja na Enyimba kucheza nyumbani italazimika kushinda pambano hilo ambalo lilionekana kuwa itakuwa mteremko kwa Enyimba huku Ittihad ikikosa pambano la nyumbani ili kujihakikishia kuvuka hatua hio itafaidika kutokana na kutopachikwa bao ktk pambano lao la mwanzo lililofutwa na Caf.

Mbali na pambano hilo la upande mmoja kutakuwa na pambano kati ya Raja Casa Blanca ya Morocco dhidi ya Asec Mimosas ya Ivory Coast ambayo pia pambano lao nchini Ivory coast halikuweza kufanyika kutokana na matatizo ya kisiasa nchini humo yaliyopelekea kiongozi wa zamani wa nchi hio kuondoshwa madarakani ambapo mpaka sasa hali sio shwari nchini humo.

mechi ngumu zaidi ni kati ya mabingwa watetezi Tp Mazembe ambao watakuwa na kibarua cha kurejesha taji lao kwa kupambana na Widad Casa Blanca ya morocco ambapo Widad Casa Blanca walishinda bao 1-0 mjini casa blanca.

National El Ahly ya Misri v/s Zasco ya Zambia ambapo mechi ya awali nchini zambia walitoka suluhu 0-0.

mapambano mengine ni kama ifuatavyo.

Group Desportivo Inter Clube 1-1 Moloudia Club d'Alger mechi ya awali.
Moloudia club d'Alger v/s G.D Inter Clube (1-1)

E.S.T 5-0 Asc Les Jaraafs
Asc Les Jaraafs v/s E.S.T (0-5)

El Hilal 1-0 Club Africain
Club Africain v/s El Hilal (0-1)

Coton Sports de Garoua V/S E.S De Setif pambano la Awali ambapo lile la marejeano litafanyika tarehe 13-05-2011 E.S De Setif V/s Coton Sports de Garoua.