WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

.

.

.

.

.

.

MUDATHIR YAHYA

MUDATHIR YAHYA

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

SEIF ABDALLA "karihe"

SEIF ABDALLA "karihe"

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

www.ofaznz.net

Total Pageviews

Sunday 22 May 2011

ORLANDO PIRATES YATWAA UBINGWA

Mbingwa Wapya wa Afrika Kusini walijulikana jana wakati timu tatu zikiwania nafasi moja ya ubingwa huo huku zikiwa zinacheza mechi zao za mwisho kumaliza msimu wa ligi.
Ajax Capetown ambao walikuwa wakiongoza ligi hio kwa point mbili na waliopewa nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa huo,Kaiser Chief na Orlando Pirates zote kutoka katika mji wa soweto mjini Johannesburg.
Walikuwa ni Pirates walioweza kuondoka na furaha za ubingwa baada ya kupata habari Ajax Capetown walitoka sare na hivyo Pirates kuwa juu ya Ajax Capetown kwa idadi ya magoli ya kufunga na kufungwa,katika mechi hio ya mwisho Orlando Pirates ilishinda mabao 2-1 dhidi ya Golden Arrows wakati Ajax Capetown ilitoka sare 2-2 dhidi ya Maritzburg United huku Kaiser Chiefs ikiifunga AmaZulu mabao 2-1 lakini kutokana na matokeo mengine hayakuweza kuwasaidia kutwaa ubingwa huo tena kwa miaka 6 mfululizo.
Orlando Pirates bingwa mpya wa afrika Kusini ambapo imezawadiwa hundi ya us$1.46 million kama mshindi wa kwanza wa mashindano hayo pia kujipatia tiketi ya kucheza Caf champions League msimu ujao.