Kiungo nyota wa Oranje Football Academy Mudathir Yahya amechaguliwa kujiunga na timu ya Mkoa wa Mjini Magharibi kitakachokwenda kushiriki mashindano ya Copa Coca Cola yatakayofanyika mjini Dar es salaam kitaifa.
Kiungo huyo mshambuliaji mwenye kujiamini na anaechezesha pasi za uhakika pamoja na uwezo mkubwa wa kufunga mabao atajumuika na nyota wengine 20 kukamilisha kikosi hicho cha vijana watakaoshiriki mashindano hayo mwaka huu 2010.
kwa niaba ya Uongozi na Wachezaji wa Oranje Football Academy unamtakia nyota huyo mafanikio mazuri.
......................................................................................................................................
......................................................................................................................................