Baada ya kusubiri miaka mitatu bila ya Ubingwa timu ya Celtics yenye makao makuu yake mjini Glasgow nchini Scotland imetwaa ubingwa wa nchi hio baada ya kuiadhibisha Kilmarnock nyumbani kwao jumla ya mabao 0-6 .
Celtics ilionyesha dhamira ya kutwaa ubingwa huo katika dakika ya kwanza tokea kuanza kwa pambano hilo ambapo walitawala mchezo hadi mwisho wa pambano hilo.
Nyota kutoka Kenya Wanyama hakucheza pambano hilo baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu wiki iliyopita dhidi ya mahasimu wao wakubwa Glasgow Rangers ambapo Rangers ilishinda kwa mabao 3-2.
Celtics ambao mashabiki wake waliufunika uwanja katika pande zote mbili za magoli pamoja na kujaza nusu ya jukwaa kuu na kuonekana kama vile wanachezea nyumbani na kuwaacha mashabiki kiduchu wa timu ya nyumbani ya Kilmarnock kupwaya na kuonekana kama hawapo kiwanjani kuishangilia timu yao ya nyumbani.
Mabao ya Celtics Rangers yalifungwa na Mulgrew dakika za 8, 35,Loovens 17,Hooper 45, 90
na Ledley katika dakika ya 88.
Executive Board begins with a focus on the new UNICEF Strategic Plan,
2018–2021
-
NEW YORK, United States of America, 7 February 2018 – The UNICEF Executive
Board opened its first regular session yesterday, welcoming its new
President fo...
7 years ago