WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

.

.

.

.

.

.

MUDATHIR YAHYA

MUDATHIR YAHYA

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

SEIF ABDALLA "karihe"

SEIF ABDALLA "karihe"

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

www.ofaznz.net

Total Pageviews

Friday 12 June 2009

ORANJE FOOTBALL ACADEMY KUIPEPERUSHA BENDERA YA TANZANIA BARANI ULAYA PAMOJA NA DUNIANI KWA UJUMLA

Moja ya mechi za O.F.A (pichani) wakipasha joto kabla ya kuanza kwa pambano.
-------------------------------------------------------------------------------------------------
Waandishi wa habari wa TV kutoka nchini Turkey TRT INTERNATIONAL wakichukua Programme jana katika viwanja vya mnazi mmoja Oranje Football Academy walikuwa wakifanya mazoezi yao kulingana na ratiba ya kocha wao ambapo leo walifanya mazoezi mepesi katika ufukwe wa maisara
-------------------------------------------------------------------------------------------------
Waandishi wa habari wa TV TRT INTERNATIONA kutoka mji wa Istanbul-Turkey wakichukua matukio ya vijana wa Oranje Football Academy jana
-------------------------------------------------------------------------------------------------
vijana wenye skills za hali ya juu wa o.f.a wakiwa katika ufukwe wa Maisara leo asabuhi ambapo pia walifanya programme ya TV TRT INTERNATIONAL
-------------------------------------------------------------------------------------------------
mchezaji wa o.f.a akiwa katka mazoezi leo asubuhi katika ufukwe wa maisara
-------------------------------------------------------------------------------------------------



ORANJE FOOTBALL ACADEMY KUIWAKILISHA TANZANIA KATIKA TV BARANI ULAYA



Amsterdam:The Netherlands



Oranje Football academy ya Tanzania imeanza kuOnyesha maendeleo yao ambapo jana na leo waliweza kuchukua TV programme maalum ya soka kwa vijana nchini Tanzania,

programme ambayo ilichukuliwa na waandishi wa habari wa TV kubwa nchini Turkey,

TV hio iitwayo TRT INTERNATIONAL ambayo mbali na kuonekanwa na watu millioni 80 wanaiishi nchini Turkey pia huoneshwa nchi karibu zote za barani ulaya pamoja na duniani kwa ujumla,katika maandilizi yaliyofanywa na viongozi wa O.F.A waliopo Europer kwa kushirikiana na wale wenzao waliopo nchini Tanzania wameweza kuwavutia waandishi wa habari hao na kutoaamini machoni mwao kwa yale waliyoyaona kutoka kwa vijana hao wa O.F.A kuwa na skills ambazo hawakutarajia kuziona hapo Tanzania,


kutokana na hali hio ambayo iliwavutia jana waandishi hao wa habari waliomba kuchukua Tv tena asabuhi ya leo ili kuweza kukamilisha programme ambayo jana waliagizwa kuifanya kutoka kwa klabu mbili kubwa za mjini Istanbul,


waandishi hao wa habari ambao waliwasiliana na wenzao wa Turkey kwa simu baada ya kuona vipaji vya vijana wa O.F.A ,tayari timu zote mbili leo zimeongea kwa njia ya simu na kiongozi wetu wa O.F.A aliyefatana na waandishi hao kuja nchini ndugu Nasa Turkey na tunatarajia karibuni tutaanza kupeleka wachezaji wetu wa O.F.A sehemu mbali mbali barani ulaya,ambapo tayari baadhi ya wachezaji wamepewa nafasi kubwa kupitia kwa waandishi hao wa habari,ambapo vilabu hivyo vitawachukua wachezaji hao kutokana na video ambayo wanazisuburi kwa hamu kwa vilabu vyote viwili kwaujumla,


O.F.A inakuwa ni klabu ya kwanza nchini kuonekanwa barani ulaya na hii itapelekea kuitangaza Tanzania kimataifa katika soka hususan kwa vijana apambo hivi sasa Tanzania imepania kuimarisha soka kwa vijana tofauti na miaka ya nyuma,ni habari njema kwa kocha wa Taifa MAXIMO na kwa Taifa zima kwa ujumla,


kutokana na kuitangaza soka ya Tanzania barani ulaya na duniani kwa ujumla O.F.A itaweza kuiwakilisha na kubeba bendera ya Taifa na kuifanya iwe nchi inayojulikana kupitia kwa vijana hawa wenye vipaji vya hali ya juu wa O.F.A,


hii ni katika mikakati ya kuinua soka laTanzania kwa kuipatia soko Ulaya ,viongozi wa O.F.A watapeleka tena nchini muda mfupi ujao waandishi wa habari wengine wa TV SBS6 moja ya TV kubwa nchini Holland ambayo huonekanwa katika bara la ulaya kwa ujumla,


pia tayari viongozi wa O.F.A wameanza mazungumzo na Tv nyingine kutoka nchini Nothern Ireland ambapo ni mpango maalum unaondaliwa kwa kitaalamu na viongozi wa O.F.A waliopo nje ili kuweza kuitangaza Tanzania kisoka barani ulaya,


Kutokana na utafiti uliochukuliwa na viongozi wa O.F.A waliopo ulaya wamegundua kuwa soka nchini Tanzania kwa vijana ni kubwa na kiwango cha hali ya juu kama vijana wakipewa nafasi kwenda nje kutokana na umri wao,tofauti na wachezaji wenye umri mkubwa ambapo viwango vyao hua tayari vimeshuka kutokana na majukumu mengi ya kimaisha,ngono,anasa na mengineyo,


tunatarajia mafanikio mazuri kwa Tanzania katika kukuza soka kwa vijana ili tufikie pale ambapo tanapostahili kufikia.na tunatarajia vilabu vingine nchini vitafata nyayo za ORANJE FOOTBALL ACADEMY
-------------------------------------------------------------------------------------------------