WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

.

.

.

.

.

.

MUDATHIR YAHYA

MUDATHIR YAHYA

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

SEIF ABDALLA "karihe"

SEIF ABDALLA "karihe"

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

www.ofaznz.net

Total Pageviews

Saturday 29 May 2010

KIUNGO WA ORANJE FOOTBALL ACADEMY AANZA MAZOEZI MEPESI


(kiungo wa Oranje Football Academy Mudathir Yahya katikati akiwa mazoezini ufukweni)




Kiungo wa kitumainiwa wa Oranje Football Academy Mudahir Yahya ameanza mazoezi mepesi na tayari amezidi kurejea katika hali yake ya kawaida baada ya kuugua na kulazwa katika hospitali ya Mnazi Mmoja jumatano iliyopita kutokana na matatizo ya tumbo.

Nyota huyo wa Oranje Football Academy ambae msimu uliopita alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mashindano ya knock-out U/17 anaendelea vizuri na mazoezi mepesi na kesho anatarajiwa kuwemo katika kikosi cha vijana wa U/17 watakapokuwa kiwanjani kupambana na Kipago F.c (tunapenda kusahihisha jina la vijana wa Kipago ambapo hapo awali lilikuwa likisomeka Kipigo f.c, jina sahihi ni Kipago f.c)

Bado haijaeleweka vizuri kama nyota huyo ataanza katika pambano hilo la kesho dhidi ya kipago f.c au ataweza kuwa katika banch ,hio itatokana na walimu wa Oranje Football Academy watakavyoweza kuamua kutokana na hali ya nyota huyo kama ataweza kumudu dakika zote za pambano hilo au dakika ngapi ataweza kucheza ili kuiweka hali yake kurejea taratibu kama kawaida.
....................................................................................................................................................................