Oranje Football Academy leo katika mfululizo wa mashindano ya kombe la Knock-out imeweza kuifunga timu ya Stone Town jumla ya mabao 2-0 katika pambano lililochezwa mapema katika kiwanja cha Mao Tse Tung.
Wafungaji katika pambano hilo ni mshambuliaji hatari Yussuf Miraji aliepachika bao moja na Yussuf Abdalla pia aliweka bao moja.
Kwa matokeo hayo ya leo Oranje Football Academy U/17 wameingia robo fainali ya mashindano hayo ambapo kesho ratiba ya timu zitakazo fanikiwa kuingia robo fainali itatolewa na kujua Oranje Football Academy itaingia kiwanjani na itapambana na timu gani katika robo fainali.
.....................
Kesho katika kiwanja cha Mchangani Malindi U/14 wa Oranje Football Academy watajitupa kiwanjani kupambana na vijana wa Villa Real katika pambano litakalofanyika saa 9 jioni.
.........................................................................................................................................................................