Oranje Football Academy jumamosi wiki hii itafanya ziara ya kwenda Nungwi kusherehekea ubingwa wa Zanzibar WA u20 ulioutwaa hivi karibuni.
Wakiwa Nungwi Mabingwa hao watacheza pambano la kirafiki na timu ya Kombaini ya Wilaya ya Kaskazini A ambapo pia watapata fursa ya kumzawadia mchezaji bora wa msimu uliomalizika utaratibu ambao unafanywa na kituo hicho cha kukuza soka kwa vijana nchini kila baada ya msimu kumalizika.