Katika pambano hilo vijana wa O.F.A walitawala mchezo kwa kutandaza soka ya uhakika na kuwapa wakati mgumu wapinzani wao hivyo kuwafanya mabingwa hao kutoka na ushindi kwa mara ya pili mfululizo katika mechi zao mbili za ligi walizocheza.
Mabao yote mawili ya O.F.A yalipachikwa kimiani na mshambuliaji wao hatari ambae pia ni mshambuliaji wa timu ya Taifa ya Zanzibar U17 Yunus Bernad na kuwahakikishia Mabingwa hao kutoka na Point 3 muhimu hivyo kujikusanyia jumla ya point 6 katika mechi mbili za ligi walizocheza.