wakiwa huko wataweza kutembelea sehemu mbali mbali za kitalii na kihistoria pamoja na kucheze mechi ya kirafiki na Timu ya soka ya Daraja la pili ya Aluta ya mji huo wa Manga Pwani,kutokana na timu hio ya Aluta kuwa timu ngumu na yenye wapenzi wengi katika mji huo tunatarajia mchezo wa kesho utakuwa na upinzani mkali na kutoa burudani safi kwa wapenzi wengi watakaofurika kuziona timu hizo mbili zikipambana kwa mara ya kwanza katika historia,hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa vijana wa Oranje football academy kufanya ziara kama hio ambapo itaweza kuwajenga vizuri chipukizi hao kisaikolojia,ambapo ziara njingi zitafatia ndani na nje ya nchi katika siku sijazo,kutokana na mipango mahiri inayofanywa na viongozi wao ni kuhakikisha chipukizi hao wanakuwa ni wawakilishi wazuri wa Taifa kwa kuwapeleka chipukizi hao katika vilabu mbali mbali nje kwaajili ya trials,na kujiunga na timu za huko kwa manufaa ya Taifa hapo baadae.
-------------------------------------------------------------------------------------------------