WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

.

.

.

.

.

.

MUDATHIR YAHYA

MUDATHIR YAHYA

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

SEIF ABDALLA "karihe"

SEIF ABDALLA "karihe"

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

www.ofaznz.net

Total Pageviews

Wednesday 1 July 2009

TANZANIA YAPANDA KIWANGO CHA SOKA DUNIANI HADI NAFASI YA 97 BAADA YA KUIFUNGA "ALL WHITES" MWEZI ULIOPITA

Tanzania imepanda kiwango cha soka duniani kutoka nafasi ya 109 hadi kufikia nafasi ya 97,
hii ni habari njema kwa Taifa katika mwezi huu wa 07-2009,Tanzania imeweza kupanda ngazi 12 juu yake kutoka katika nafasi iliyokuwepo kabla ya tarehe 03-06-09 nafasi ya 109, hii inatokana na kushinda mechi ya mwisho ya kirafiki kati yake na New Zealand kwa mabao 2-1 katika kiwanja cha taifa-dar es salaam, kutokana na ushindi huo hivi sasa Tanzania itakuwa na kiwango bora cha soka duniani zaidi kuliko New Zealand yenyewe ambao hivi sasa wapo katika nafasi ya 100 duniani kwa mujibu wa Fifa world Ranking iliyotoka leo, hii itapelekea furaha kubwa kwa Watanzania pamoja na kocha Maximo,kabla ya mechi ya stars /New Zaland, "all Whites" walikuwa wana kiwango bora ukilinganisha na stars,kutokana na kiwango cha Tanzania kupanda hii inaonyesha kuwa Tanzania inahitajia mechi nyingi za kirafiki na timu zenye kiwango kizuri duniani kwani inapelekea kuipandisha rank kubwa ya kisoka duniani pindipo Stars wakishinda mechi hizo,
kwamaana hio Tanzania itakua inashika nafasi ya 3 kwa soka kwa nchi za Africa mashariki na Kati ikitanguliwa na Uganda nafasi ya 75,sudan 91,Tanzania 97,mabingwa wa CHAN 2009 D.R. Congo wanashika nafasi ya 102,Ethiopia 138,Kenya pamoja na kuwa wanashriki katika world cup qualification wanashika nafasi ya 105,malawi 110,Rwanda ambao kiwango chao cha soka kwa miaka mingi kilikuwa ni bora kuliko Tanzania wanashika nafasi ya 113,Washiriki wa Fainali za kombe la dunia zilizopita 2006 zilizofanyika ujerumani -Angola wanashika nafasi ya 103,
kuna mlolongo wa timu za Europer ambazo Tanzania inakiwango kikubwa cha soka duniani kama vile Georgia 104,Luxamburg 119,Montnegro 98, hii inaonyesha Kiwango cha Tanzania kimepanda sana kutokana na kuwafungwa mabingwa wa Oceania "All Whites" mwezi uliopita na inatakiwa Tanzania ijiamini kuweza kuagizia na kwenda kucheza mechi na timu kubwa kwa nchi za bara la ulaya ili kuweza kuipandisha kiwango zaidi nchi pamoja na kuweza kuwatanga wachezaji wetu nje,tunatarajia pia kutokana na ligi kuu Tanzania kutawaliwa na wachezaji wa kigeni itapelekea kuongeza viwango vya soka nchini na tunatarajia katika miaka michache inayofata Tanzania itakuwa ni nchi ya pili kwa ligi bora kwa nchi za Africa mashariki na kati pamoja na kusini mwa Africa baada ya south Africa ambapo wachezaji wengi wa Africa wamekuwa wakikimbilia huko kwa miaka mingi kwenda kucheza soka,
Hongera Taifa stars, Honger Watanzania kwa ujumla.
------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------------
------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------------