katika mchezo huo wa leo ambao vijana a O.F.A walitawala katika vipindi vyote viwili waliweza kuwafunza soka wenyeji wao hao wa Fujuni baada ya kutandaza kandanda safi na kuwaburudisha watazamaji waliofika kuona pambano hilo,
kutokana na soka ya kufundishwa iliyoonyeshwa na chipukizi hao wa O.F.A waliweza kutawala mchezo huo katika wizara zote,
wakiongelea mchezo wa leo baada ya kumalizika kwa pambano hilo viongozi wa klabu ya Fujoni Stars ambao wapo katika daraja la pili kwapamoja walisema "vijana wa O.F.A ni wazuri sana,wametuzidi sana kiwanjani,na hatukuwahi kupambana au kuona timu yoyote hapa nchini kucheza soka kiwango ambacho hawa vijana wa O.F.A leo wametuonyesha hapa katika kiwanja chetu,"
O.F.A inatarajia kucheza mechi nyingine mwishoni mwa wiki ijayo na vijana wanatarajiwa
kuendeleza kuonyesha soka safi na kushinda mchezo huo ambayo ni matayarisho kwaajili ya msimu ujao wa ligi.ambapo itafatia michezo mingine pia ya kirafiki kwaajili ya kukinoa kikosi kipya cha chipukizi hao machachari wa O.F.A