makamo wa rais wao anaeishi nothern Ireland Mudathir vile vile waliweza kutambulishana na kiongozi wao raia wa Holland Den Heijer,
katika kikao hicho ambacho waliweza kuzungumzia mambo mengi ya maendeleo ya kituo hicho cha kukuza soka kwa vijana mambo ambayo yatawawezesha kufikia malengo yanayokusudiwa kifikia,
mbali na maongezi hayo pia waliweza kukabidhiwa baadhi ya vifaa vya michezo ambapo ni mwanzo wa kupata vifaa kwa kituo hicho ambapo vifaa hivyo ni kutoka kwa viongozi wao wa holland,
baada ya kikao hicho ambacho kiliweza kuleta muamko mpya kwa viongozi na wachezaji wa O.F.A ambapo hata hivyo waliweza kuwakosa viongozi wao wawili ambao hawakuhudhuria kutokana na kubanwa na shughuli mbalimbali za kikazi.
Mara baada ya kikao hicho jioni waliweza kupata futari ya pamoja ambapo viongozi na wachezaji hao kwa pamoja waliweza kujumuika kwa mara ya kwanza na viongozi wao kutoka ulaya katika futari hio tokea kuanzishwa hivi karibuni kwa kituo hicho cha kukuza soka kwa vijana .
-------------------------------------------------------------------------------------------------