WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

.

.

.

.

.

.

MUDATHIR YAHYA

MUDATHIR YAHYA

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

SEIF ABDALLA "karihe"

SEIF ABDALLA "karihe"

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

www.ofaznz.net

Total Pageviews

Thursday 17 September 2009

ORANJE FOOTBALL ACADEMY KUPATA FUTARI LEO PAMOJA NA KUTAMBULISHWA VIONGOZI WAO KUTOKA NJE

(Wachezaji wa O.F.A wakiwa na nyuso za furaha kwenda kuchukua Kombe na zawadi zao mara baada ya fainali ya knock-out ambapo walitwaa ubingwa huo).

-------------------------

Kituo cha kukuza soka kwa vijana cha ORANJE FOOTBALL ACADEMY leo mchana watakutana kwa mara ya kwanza na viongozi wao kutoka nje na kutambulishana pamoja na kuzungumzia mambo mengi ya maendeleo ya kituo hicho cha O.F.A.
ambapo hivi sasa itakuwa inaingia katika hatua ya pili ambapo msimu iliomalizika ilianzia kwa kuwa na mafanikio mazuri sana.

katika kikao hicho wachezaji wote na viongozi wa O.F.A wataweza kukutana na makamo wa rais wa O.F.A Mudathir anaeishi Belfast-Nother Ireland(Mudathir ndie ambae ameifanikisha safari ya Rivaldo kwa kiasi kikubwa)

pia wataweza kukutana na mwandishi na mpangaji wa shughuli za kituo hicho raia wa holland Isabel Den Heijer ambae ataweza kukabidhi baadhi ya vifaa kwa vijana hao O.FA ikiwa na hatua ya kwanza katika kukiendeleza kituo hicho cha O.F.A.

mbali na viongozi hao wataweza kukutana na kiongozi wao mwingine kwa mara ya kwanza ambae ana wadhifa wa juu katika chama cha soka cha Tanzania TFF(jina litatolewa baadae)

mara baada ya kikao hicho kinachotarajiwa kufungua zaidi mwangaza wa maendeleo kwa vijana hao wenye sifa ya kutandaza soka ya kileo na wenye vipaji vya hali ya juu kutakuwa na Futari iliyoandaliwa na O.F.A kwa ajili ya viongozi,na wachezaji wote wa kituo hicho cha ORANJE FOOTBALL ACADEMY.
-------------------------------------------------------------------------------------------------