akiongea na kiongozi wa O.F.A anayeishi Holland nyota huyo Rivaldo alisema "Nashukuru sana safari haikuwa na matatizo yoyote,nimefika salama"
nyota huyo wa kimataifa mwenye asili ya Kitanzania ambae kwa kawaida huiwakilisha nchi yake Mozambique kwa timu za taifa za U-18, U-20 pamoja na timu kubwa ya taifa ya nchi hio atakuwa na mapumziko ya siku mbili ambapo ataweza pia kuona mechi ya ligi ya timu yake ambao watacheza mwishoni mwa wiki nyumbani,
jumatatu Rivaldo ataanza mazoezi rasmi na klabu yake hio ya Belfast.
akiongea kwa nja ya simu kutoka Belfast manager wa klabu ya BANGOR F.C mr COLLIN akiwa na furaha aliwashukuru viongozi wa O.F.A kwa kufanikisha ujio wa nyota huyo mwenye umri wa miaka 18.
RIVALDO amepata nafasi ya kwanza kutoka katika kituo cha kukuza soka kwa vijana cha ORANJE FOOTBALL ACADEMY ambao katika mikakati yao ni kutoa wachezaji wengi chipukizi kwenda kucheza soka ya kulipwa nje.
-------------------------------------------------------------------------------------------------