Chipukizi wa Oranje U-19 leo waliendeleza ubabe wao katika ligi baada ya kuitandika timu ya New Boko kwa jumla ya mabao 3-0.
katika mechi hio ambayo vijana wa O.F.A walionekana kuelewana na kuzidisha ufundi wa kusakata soka siku hadi siku zinavyoendelea waliweza kupachika mabao hayo kupitia kwa mshambuliaji wao hatari Seif Abdalla (karihe) X 2, na mshambuliaji mwingine chipukizi mwenye uwezo mkubwa katika safu hio ya ufungaji Yussuf Abdalla (mido)
...........................................................................................................................................................................
Vijana wadogo U-14 wa Oranje Football Academy leo wamepoteza mechi baada ya kufungwa na Valencia bao 1-0 katika mchezo mkali na wakusisimua ambapo vijana wa O.F.A walikosa nafasi nyingi za kuweza kusawazisha bao na hata kuweza kutoka na ushindi katika mechi ya leo.
...........................................................................................................................................................................