Mabingwa wa soka wa Europer League,mabingwa wa ligi Portugal,mabingwa wa kombe la chama cha soka portugal(FA) kama Fc Porto haitoshi imetwaa ubingwa mwingine baada ya kuichapa bila huruma Victoria Guimaraes 6-2 katika pambano la fainali la Portuges cup lililofanyika jana ambapo mabingwa hao walionyesha uwezo mkubwa msimu huu katika soka barani ulaya.
pamoja na kudaiwa kama kocha wao yupo katika hatua ya kunyakuliwa na timu kadhaa za bara hilo la ulaya,kutokana na mafanikio makubwa F.C Porto waliyoyapata msimu huu wameahidi kutofanya makosa kama waliyoyafanya miaka iliyopita kumuachia kocha wake Mourinho,pamoja na nyota kadhaa akiwemo Deco,Carvalho na wengine kuihama timu hio hivyo kuigharimu muda timu yao kuijenga upya msimu huu.
katika list ambayo magezeti ya uingereza yameripoti kocha wa F.c Porto Andre Villas-Boas ni mmoja kati ya majina ya makocha kadhaa waliopendekezwa katika timu ya Chelsea f.c ya London.
Kutokana na matokeo hayo ya jana Fc Porto ni timu pekee ya barani ulaya iliyotwaa makombe yote timu hio iliyoshiriki msimu mmoja kwa mwaka huu 2011.
Executive Board begins with a focus on the new UNICEF Strategic Plan,
2018–2021
-
NEW YORK, United States of America, 7 February 2018 – The UNICEF Executive
Board opened its first regular session yesterday, welcoming its new
President fo...
6 years ago