WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

.

.

.

.

.

.

MUDATHIR YAHYA

MUDATHIR YAHYA

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

SEIF ABDALLA "karihe"

SEIF ABDALLA "karihe"

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

www.ofaznz.net

Total Pageviews

Friday 27 January 2012

IVORY COAST YATINGA ROBO FAINALI

Ivory Coast imekuwa ni nchi ya pili kitinga katika hatua ya Robo fainali baada ya kuifunga Bukina Faso jumla ya mabao 2-0 katika pambano lao la pili katika kundi B.
Mabao ya Ivory Coast yalifungwa na kalou katika dakika ya 16 wakati lile la pili lilipachikwa na mlinzi mahiri wa Bukina Faso Bakari Kone aliyejifunga mwenyewe kwa kichwa katika harakati za kuokoa katika dakika ya 82.
Ivory Coast imejikusanyia jumla ya point 6 katika michezo miwili waliyocheza na kushinda yote huku Bukina Faso waliobakia mechi moja dhidi ya Sudan wakiyaaga mashindano hayo baada ya kufungwa mechi ya awali jumla ya mabao 2-1 dhidi ya Angola hata kama watashinda pambano lao la mwisho dhidi ya Sudan.
Katika pambano jingine la kundi hilo Sudan ilitoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya Angola hivyo kuwa na matumaini ya kusonga mbele kama itaifunga Bukina Faso katika pambano lao la mwisho la kundi hilo na pia kuiombea dua mbaya Angola ifungwe na Ivory Coast.
Mabao ya Sudan katika pambano hilo yote yalifungwa na Bashir katika ya 33 na 74 wakati yale ya Angola pia yalifungwa na Manucho katika dakika ya 5 na dakika ya 50 kwa njia ya penalti