WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

.

.

.

.

.

.

MUDATHIR YAHYA

MUDATHIR YAHYA

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

SEIF ABDALLA "karihe"

SEIF ABDALLA "karihe"

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

www.ofaznz.net

Total Pageviews

Wednesday 1 February 2012

MALI YAIFUNGA BOTWANA NA KUINGIA ROBO FAINALI

Mali imeifunga Botswana 2-1 katika pambano lao la mwisho na kujihakikishia kucheza robo fainali ya Can 2012 baada ya Guinea ambao pia walikuwa na nafasi ya kusonga mbele kutoka sare ya 1-1 na Ghana hivyo Guinea imeyaaga mashindano hayo kama mshindi wa tatu wa kundi hilo na Botswana kushika nafasi ya mwisho.

Mabao ya Mali yalipachikwa na Dembélé kwa bao la kusawazisha katika dakika ya 57 baada Botswana kutangulia kufunga bao katika dakika ya 51 bao lililofungwa na Ngele,Keita iliipatia Mali bao la pili katika dakika ya 75 bao ambalo lilitosha kuwasukuma Mali katika hatua ya robo fainali huku wakiungana na Ghana ambao ni washindi wa kwanza wa kundi hilo.
Ghana ilitangulia kufunga bao lao katika dakika ya 28 bao lililotundikwa kiufundi na Badu kwa mpira wa kuungani nje ya sanduku la goli la Guinea wakati lile la Guinea lilifungwa kupitia kwa Camara katika dakika ya 45 iliyechonga krosi pembeni kushoto ambayo iliyokwenda moja kwa moja wavuni.