WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

.

.

.

.

.

.

MUDATHIR YAHYA

MUDATHIR YAHYA

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

SEIF ABDALLA "karihe"

SEIF ABDALLA "karihe"

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

www.ofaznz.net

Total Pageviews

Tuesday 7 February 2012

NEW "FORLAN" CRISTIAN TELLO

Tello ikimtoka beki wa Real Socidade mwoshoni mwa wiki iliyopita katika uwanja wa Camp nou
......................................................................................................................................


Tello alipongezwa baada ya kupachika bao la kuongoza kwa BArça dakika ya 19.

.......................................................................................................................................

F.c Barçelona wamefungua kifaa kipya kutoka timu B ambaye juzi alingára sana katika mechi yake ya pili tokea kupandishwa katika timu A.baada ya kucheza dakika chache za mwisho pambano la Copa Del Rey dhidi ya Valencia Nyota huyo mpya anaevalia jezi namba 37 ambao alikuwa akivaa jezi namba 7 katika timu B aliwanyanyasa mabeki wa Valencia hivyo kumshawishi kocha Guardiola kumpanga katika pambano lake la mwanzo la La Liga dhidi ya Real Sociedad.


Ilimchukua nyota huyo mpya Tello dakika 19 tu za kipindi cha kwanza kuandika bao la kwanza kwa timu yake na bao lake la kwanza tokea kuanza kuchezea timu kubwa ya Barçelona.Nyota huyu mwenye umri wa miaka 20 anasifa kama ambazo Diego Farlan alivyokuwa hivyo kutokana na uwezo mkubwa alioonyesha pamoja na kujiamini sana katika ushambuliaji pembeni kushoto akishirikiana na Messi pembe kulia inaonekana kutakuwa na kazi kubwa kwa mabeki wa timu pinzani kuweza kuwadhibiti nyota hao wawii ambapo pia Messi alipikwa huko chini katika timu B kabla ya kuja kuonyesha makali yake katika timu A.


Sat 27 Aug timu za Barçelona B na Villareal B zilicheza katika ligi ya Segunda Div ,Villareal B ilishinda 2-0 daraja moja tu kutoka La Liga ambapo hapo wachezaji hupikwa na kupambana na timu zote zinazoshuka daraja la pili kutoka La Liga na Zile zinazopanda La Liga kwa vile timu hizo haziruhusiwi kupanda daraja kutokana na kaka zao kuwa katika madaraja hayo lakini inakuwa wachezaji wamewiva tayari kucheza katika timu kubwa wakati wowote pia kuzisaidia timu za taifa za vijana za nchi hizo,


Hapa nchini TFF na ZFA inashindwa kuzisimamia timu kubwa au timu zenyewe zinashindwa kuwa na mfumo mzuri wa kuwatengeneza vijana wenyewe kwa bei nafuu na kuwa na viwanda vya kuzalisha nyota wao na kutegemea mfumo wa kununua wachezaji kutoka katika timu nyingine au kutoka nje mfumo ambao miaka yote tokea kuanzishwa timu hizo hakujaleta mafanikio yoyote katika timu hizo zaidi ya kucheza soka katika magazeti.



Hivi sasa Fc Barcelona B inashika nafasi ya 3 katika msimamo wa ligi hio yenye timu 22 nyingi zikiwa zimewahi kucheza ligi daraja la juu la Liga hivyo kufanya kila nyota wa FC Barçelona anaepandishwa kuwa mkali kama Xavi,Eniesta na karibuni timu nzima hivyo kuifanya timu hio kununua mchezaji 1 au wawili tu kwa kila msimu kutokana na kuwatengeneza wachezaji wenyewe kwa stail wanayotaka kuja kuichezea katika timu kubwa.


Kutokana na usimamizi m'bovo kwa bahari timu zinazoshiriki ligi kuu ya Vodacom wanashiriki ligi ya uhai cup mwezi mmoja tu na miezi 11 wanafanya mazoezi tu na hata bila kupewa mechi katika timu kubwa ili kuwajenga wachezaji hao ambao ndio nyota wa taifa la baadae.


kuna ligi mbalimbali za madaraja mbalimbali ambapo timu hizo zinaweza kushiriki ambapo zinaweza kuwafanya wachezaji hao kushiriki katika hali ya kimashindano msimu mzima kuliko kusubiri mwezi mmoja wa uhai cup ambao hausaidii chochote katika soka.


vyama vya soka viwaruhusu wachezaji wote wa timu B waliosajiliwa kushiriki katika timu A wakati wowote wakihitajika kutumiwa na wilabu hivyo katika timu kubwa ili kuongeza ushindani kwa wachezaji hao huko chini kwa kila mmoja wao kuwania nafasi ya kuitwa timu kubwa wakati wowote ndani ya msimu mzima wakati ligi ikiendelea.Nadhani imefika wakati sasa soka ya Tanzania kubadikika vinginevyo tutakuwa tunaangalia nchi ndogo za Africa zikicheza katika Tv kutokana na mfumo wetu wa soka uliopitwa na wakati.


Aidha vilabu vikubwa vinavyojiita Sports Clubs,lini vitaanzisha michezo mingine ili jina lao likamilike la kujishighulisha na Sports katika timu zao kama wanashindwa kuwa na timu za watoto zenye kusimamiwa vizuri na kuleta mapinduzi ya soka nchini.