WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

.

.

.

.

.

.

MUDATHIR YAHYA

MUDATHIR YAHYA

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

SEIF ABDALLA "karihe"

SEIF ABDALLA "karihe"

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

www.ofaznz.net

Total Pageviews

Monday 6 February 2012

ZAMBIA VS GHANA,IVORY COAST VS MALI NUSU FAINALI CAN



Ghana imeitoa Tunisia nje ya michuano ya Afcon na kuifanya michuano hio kwa miaka mingi kuingia hatua ya nusu fainali bila ya nchi yoyote kutoka North Africa baada kuifunga mabao 2-1 katika pambano lililochezwa kwa muda wa dakika 120 baada ya kutoka sare ya 1-1 katika dakika 90 za kawaida.Ghana ilitangulia kufunga bao la kwanza katika dakika ya 10 bao lililotumbukizwa kwa kicha na nahodha wao Mensah,Tunisia ilisawazisha bao hilo katika dakika ya 42 bao lililofungwa na Khalifa hadi kumalizika dakika 90 za kawaida mabao yalikuwa ni 1-1,


Kipa wa Tunisia Mathlouthi aliwazawadia Ghana bao la ushindi baada ya kuutema mpira wa krosi uliomkuta Andre Ayew katika dakika ya 101 aliepachika bao hilo kirahisi na kutosha kuipeleka nchi katika hatua ya nusu fainali ambapo sasa itakubwana na Zambia na Ivory Coast itacheza na Mali ambayo mapema iliwatoa wenyeji wa mashindano hayo Gabon kwa njia ya penalti baada ya kutoka sare 1-1 katika dakika 120 za pambano hilo.


Penelti za Gabon zilifungwa na Poko,Mbanangoye,Mouloungui,Aubameyang alipoteza penalti baada ya kipa wa Mali Diakite kuokoa penalti hio na Manga aliifunga penalti ya mwisho.


Mali walipachika wavuni penalti zote 5 kwa mikwaju iliyopigwa na Diabate,Yatabare,Kante,Traore na Keita kumalizia penalti ya mwisho hivyo Mali sasa itakunana na Ivory Coast katika nusu fainali ya pili.