WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

.

.

.

.

.

.

MUDATHIR YAHYA

MUDATHIR YAHYA

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

SEIF ABDALLA "karihe"

SEIF ABDALLA "karihe"

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

www.ofaznz.net

Total Pageviews

Sunday 11 March 2012

TP MAZEMBE YASAJILI BEKI KUTOKA BRASIL

Mabingwa wa zamani wa Afrika Tp Mazembe mwezi januari imemsajili kwa mwaka mmoja mlinzi mkali kutoka Brasil  Julio Cesar dos Santos.
Beki huyo amesema amekuja Afrika kusaka ushindi na kutwaa mataji mengi iwezekenavyo likiwemo la ubingwa wa Mabingwa wa duniani ambao Tp Mazembe ilikuwa karibu kuutwaa mbele ya Inter Milan ya Italia miaka 2 iliyopita 2010.
Beki huyo aliongea kuwa mapenzi yake kwa Tp Mazembe yalikuja ghafla mara baada kuona mechi ya nusu fainali kati yake na International ya mabingwa wa Brasil wakati huo na Tp Mazembe kuichapa timu hio na kuingia fainali za mabingwa hao wa dunia.
Dos Santos mwenye umri wa miaka 31 anafurahia maisha ya Lubumbachi pamoja na watu wengi kuonyesha urafiki pia kufurahia chakula mjini hapo pamoja na kuwa na mandhari nzuri ya makaazi yake ambapo amesema kutoimisi sana Brasil.
Mlinzi huyo amewahi kuvichezea vilabu kadhaa nchini Brasil zikiwemo miamba ya nchi hio Sao Paulo na Vasco Da Gama.
Alizidi kusema kuwa soka ya hapo haina tofauti kubwa ukilinganisha na Brasil na kwamba Vipaji vilivyopo hapo huwezi kuamini.Kwa habari zaidi za TP Mazembe pitia katika mtandao wao hapo chini kushoto katika blog hii.