Mabingwa wa soka wa Zanzibar kwa vijana wenye umri chini ya mika 20 ORANJE FOOTBALL ACADEMY leo wameanza vyema kampeni za kutetea ubingwa wao baada ya kuilaza LEEDS UNITED kwa bao 1-0 katika pambano ambalo vijana wa O.F.A walionekana kuwa chini ya kiwango chao cha kawaida.
Pamoja na kucheza chini ya kiwango chipukizi wa O.F.A waliandika bao hilo muhimu kupitia kwa Yunus Abdalla katika mechi zinazoshirikisha timu 6 bora.
Katika mechi ya mwisho hatua ya makundi ambapo Leeds walikuwa ni washindi wa kwanza wa kundi hilo waliweza kuwafunga O.F.A jumla ya mabao 3-1 hivyo katika pambano la leo ilikuwa ni muhimu la kuanza kampeni ya kumpata bingwa wa Zanzibar kituo cha Unguja kabla ya kuwapata wawakilishi wanaozikutanisha timu kutoka kituo cha Pemba na kumpata bingwa Zanzibar ubingwa ambao hivi unashikiliwa na Vijana wa O.F.A.
Executive Board begins with a focus on the new UNICEF Strategic Plan,
2018–2021
-
NEW YORK, United States of America, 7 February 2018 – The UNICEF Executive
Board opened its first regular session yesterday, welcoming its new
President fo...
6 years ago