WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

.

.

.

.

.

.

MUDATHIR YAHYA

MUDATHIR YAHYA

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

SEIF ABDALLA "karihe"

SEIF ABDALLA "karihe"

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

www.ofaznz.net

Total Pageviews

Saturday 9 March 2013

MATOKEO YA LIGI U17 NA U14

Vijana wa Oranje Football Academy (O.F.A) U17 leo Jumamosi 9/3/2013 katika mchezo wa Round No.8 wameweza kupata ushindi wa goli 1 - 0 dhidi ya timu ya Migombani Kids. mchezo uliochezwa katika Kiwanja cha Mao Tse Tung 'B' Saa 2:00 asubuhi.
Goli la Oranje limefungwa na Mchezaji machachari Famhi Habib (Agogo) kwa shuti kali lililomshinda mlinda mlango wa Migombani Kids.
Hata hivyo vijana wa O.F.A itabidi wajilaumu kwa ushundi huo mdogo wa goli 1 baada ya kupata nafasi nyingi na kushindwa kuzitumia.
Leo jioni saa 10:30 vijana hao wa U17 watakutana mazoezini kwa ajili ya kujadili na kupanga mikakati imara ya timu hiy, huku ndugu zao wa wa U14 watakuwa wakifanya mazoezi ya pamoja na kupata nasaha kutoka kwa Uongozi Mkuu wa O.F.A.
Katika mechi za ligi za wiki iliyopita Jumamosi tarehe 2/3/2013 Saa 2:00asubuhi matokeo ni Oranje  Football Aacademy U17 ilifungwa jumla ya mabao 0 - 3 dhidi ya  New Vision.

Wakati wakubwa zao wakikubali kuchapwa ndugu zao wa O.F.A U14 waliweza kuichakaza timu ya New Znz Academy jumla ya mabao 3-1  pambano lililofanyika siku ya Jumamosi tarehe 2/3/2013 Saa 10:00 asubuhi.
Timu zote mbili zipo katika nafasi nzuri ya kusonga mbele katika hatua ya 12 Bora kwa kutafuta Bingwa wa Ligi 2012 / 2013 ambapo kila kundi linatakiwa kutoa timu nne zilizoshika nafasi za juu ya msimamo wa ligi hio katika makundi yao.
fuatilia habari za chipukizi wetu kupitia katika webblog hii inayomilikiwa na kituo chetu cha www.oranjefootballacademy.blogspot.com