WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

WELCOME "KARIBU" TO ORANGE FOOTBALL ACADEMY ZANZIBAR

.

.

.

.

.

.

MUDATHIR YAHYA

MUDATHIR YAHYA

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

SEIF ABDALLA "karihe"

SEIF ABDALLA "karihe"

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

www.ofaznz.net

Total Pageviews

Sunday 2 August 2015

ORANGE FOOTBALL ACADEMY YAIPONGEZA FC AZAM KWA KUTWAA UBINGWA WA CECAFA 2015




(Picha hizi mbili za juu ni kwaniaba ya Saleh Jembe)


Kituo cha kukuza soka kwa vijana nchini Orange Football Academy kinajumuika na Watanzania Wote nchini kuipongeza timu ya Fc Azam kwa kutwaa ubingwa wa Cecafa kwa vilabu bingwa za nchi za Afrika Mashariki na Kati huku mchezaji Mudathir Yahya alietokea katika kituo cha Orange Football Academy akiwa ni mmoja kati ya wachezaji waliochangia timu hio kuanzia mwanzo hadi kufikia hatua ya nusu fainali ya michuano hio.

Hii ni historia mpya inaandikwa na mabingwa hao wapya wa ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati hivyo kuashiria mapinduzi makubwa ya soka katika ukanda huu.

Pamoja na mashindano hayo kuonyesha kuwa yanahitaji kuboreshwa ili kuondoa mtazamo wake wa sasa ambao ni mfumo wa miaka mingi na uliopitwa na wakati katika maendeleo ya soka la nchi hizo lakini Fc Azam imewezakuonyesha mabadiliko yake binafsi na kuviamsha vilabu vingine vya ukanda huu kuiga mfano huu.

Azam FC imeifunga Gor Mahia kwa mabao 2-0 na kubeba ubingwa wa Kagame wakiwa hawajafungwa hata bao moja katika dakika 90 za kawaida za mchezo, (ukiondoa mabao ya mikwaju ya penalti kati yake na Yanga katike mechi ya robo fainali.

Mwaka 2002, Tusker ya Kenya ilifanya hivyo, lakini Azam FC imefanya hivyo huku ikiwa haijafungwa hata bao moja, Simba na Yanga hazijawahi kufanya hivyo.

Bao la kwanza la Azam FC lilifungwa na John Bocco ambaye aliipangua beki ya Gor kabla ya kupiga krosi safi kabisa iliyomfikia Bocco akamaliza kazi.


Bao la pili, likafungwa Kipre ambaye alipiga mpira wa adhabu na kipa wa Gor akadhani unatoka.

Baada ya hapo, Gor iliendelea kupambana lakini ilishindwa kuukamata mziki wa Azam FC ambao walikuwa safi huku beki Serge Wawa akimtuliza mshambuliaji hatari Michael Olunga.

AZAM FC wametwaa ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame baada ya kuifunga mabao 2-0 Gor Mahia ya Kenya katika mchezo wa fainali uliofanyia Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jioni ya leo.

Azam FC wanakuwa timu ya kwanza ya Tanzania nje ya Simba na Yanga SC kutwaa taji hilo- wakishiriki kwa mara ya tatu tu mashindano hayo baada ya mwaka 2012 walipofika fainali na kufungwa na Yanga SC 2-0 Dar es Salaam na mwaka jana kutolewa kwa penalti 4-3 mjini Kigali, Rwanda baada ya sare ya 0-0 ndani ya dakika ya 90 katika Robo Fainali na El Merreikh ya Sudan walioibuka mabingwa.
Timu hiyo yenye maskani yake Azam Complex, Chamazi, Mbade, Temeke mjini Dar es Salaam imeshinda mechi zake zote kuanzia Kundi C bila kuruhusu nyavu zake kuguswa hata mara moja- na ‘ilipata shida’ kidogo tu mbele ya Yanga SC katika Robo Fainali ilipolazimika kushinda kwa penalti 5-3 baada ya sare ya 0-0 dakika 90, wakati Nusu Fainali iliilaza KCCA 1-0.


Kwa ushindi huo, timu hiyo ya Alhaj Sheikh Said Salim Awadh Bakhresa na familia yake inazawadiwa kitita cha dola za Kimarekani 30,000 (Sh. Milioni 60), wakati Gor Mahia wanapozwa na dola 20,000 (Sh. Miliioni 40).

Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Louis Hakizimana wa Rwanda aliyesaidiwa na Nagi Ahmed wa Sudan na Suleiman Bashir wa Somalia, hadi mapumziko tayari Azam FC walikuwa mbele kwa bao hilo 1-0.
Bao hilo lilipatikana dakika ya 16, mfungaji Nahodha John Raphael Bocco ‘Adebayor’ aliyemalizia kwa kichwa krosi ya Kipre Herman Tchetche kutoka upande wa kulia.








Azam FC walitawala mchezo vizuri kwa dakika 20 za mwanzo, lakini baada ya hapo kasi yao ikapunguzwa na uchezaji wa rafu wa wachezaji wa Gor Mahia ambao hawakuchukuliwa hatua yoyote na refa Hakizimana. 

Wachezaji wa Gor walikuwa wakiwapiga viwiko na mateke wachezaji wa Azam FC na kuanguka chini wakitokwa hadi damu, lakini hiyo haikumfanya refa Hakizimana japo kutoa kadi ya njano.
Hali hiyo iliwafanya washambuliaji wa Azam waanze kucheza kwa woga na kupunguza kasi yao ya mashambulizi- huku Gor Mahia wakitumia mwanya huo nao kuanza kushambulia.
Medie Kagere alikaribia kuisawazishia Gor Mahia dakika ya 22 kama si beki muhimili wa ukuta wa Azam FC, Serge Wawa Pasacal kuokoa.
Kipindi cha pili, kocha Stewart Hall wa Azam FC alianza na mabadiliko akimtoa winga Farid Mussa Malik na kumuingiza beki David Mwantika.

Mabadiliko hayo yaliyolenga kuimarisha ulinzi yaliisaidia Azam FC kupunguza kasi ya Gor Mahia na kufanikiwa kuendelea kutawala mchezo. 
Mshambuliaji nyota kutoka Ivory Coast, Kipre Herman Tchetche akaifungia bao la pili Azam FC dakika ya 64 kwa shuti la mpira wa adhabu lililompita kama mshale kipa wa Gor Mahia, Boniphace Olouch.




Mchezo huo uliotangulia mchana wa leo, KCCA ya Uganda iliifunga 2-1 Khartoum N ya Sudan na kumaliza katika nafasi ya tatu.
Kikosi cha Azam FC kilikuwa; Aishi Manula, Aggrey Morris, Morald Said, Pascal Wawa, Farid Mussa/Erasto Nyoni dk46, Shomari Kapombe, Jean Mugiraneza, Himid Mao, Ame Ali/Frank Domayo dk69, John Bocco na Kipre Tchetche/dk88.


Gor Mahia; Boniphace Olouch, Mussa Mohammed, Sibomana Abouba, Harun Shakava, Karim Nzigiyimana, Innocent Wafula/Enock Agwanda dk83, Khakid Aucho, Godfrey Walusimbi, Medie Kagere/George Odhiambo dk83, Michael Olunga na Erick Ochieng/Ali Abondo dk74.


Hongera sana Fc Azam wachezaji,benchi la ufundi,Uongozi mzima wa klabu pamoja na Uongozi wa kampuni nzima ya Bakhresa Group kwa mchango wao mkubwa katika soka ambao umetoa ajira kwa vijana wengi ndani na nje  nchi pamoja na lengo lao la kuiletea hadhi Tanzania katika ramani ya soka barani Afrika.

Tunaamini hivi sasa nguvu zaidi zitaelekwezwa katika mashindano ya kombe la washindi wapili wa Afrika CAF. 

Tunatarajia matajiri wengine nchini watafata njayo za Azam Fc kwa maendeleo ya Taifa.







AZAM GOUP COMPANIES: --->   http://bakhresa.com/